Wananchi wa CAR wasema wanachotaka wao ni amani tu
Wakazi wa mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR wamesema wanachotaka wao hivi sasa ni amani ili waweze kuendelea na maisha yao ya kawaida baada ya miaka minne ya mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.
Wakazi hao wamesema hayo wakati wakizungumza na Idhaa ya Umoja wa Mataifa huko Bangui, mji mkuu wa CAR wakati huu ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres anatarajia kuanza ziara Kesho Jumanne.
Amesema hivi sasa biashara inashamiri lakini mashambulizi dhidi ya waislamu ni lazima yakome kwani wanachotaka wao ni amani na maridhiano.
Bwana Ismael ameshutumu vikosi vya serikali kwa kutotilia maanani ulinzi wao huku akipongeza ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini humo MINUSCA kwa kuwapatia ulinzi.
Wakati wa mapigano moja ya daraja jijini Bangui ambalo lilijulikana kama daraja la kifo lililikuwa ndio mstari wa mapigano kati ya pande kinzani na sasa kuna amani na limepatiwa jina la daraja la Yakite likitumika kusafirisha abiria na mizigo bila hofu yoyote.
Kesho Katibu Mkuu Guterres pamoja na kutumia ziara yake kuadhimisha siku ya Umoja wa Mataifa, atatoa shukrani na kukumbuka walinda amani 12 waliouawa nchini humo tangu mwezi Januari mwaka huu wakilinda raia.
Naye Mkuu wa kikosi cha MINUSCA Luteni Jenerali Balla Keita amesisitiza kuwa kamwe hakuna suluhu ya mzozo huo wa CAR kwa njia ya kijeshi bali kisiasa na kikosi chake kinasaidia kuweka mazingira bora ya ulinzi na usalama.