Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakimbizi na wahamiaji waendelea kushikiliwa mateka Libya

Wakimbizi na wahamiaji waendelea kushikiliwa mateka Libya

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, linaendelea na jitihada za kusadia mahitaji ya dharura kwa  wakimbizi zaidi ya 14,500 wanaosadikiwa kutekwa na magenge ya wahalifu katika maeneo mbalimbali ya mji wa Sabratha huko Libya .

Bwana  Andrej Mahecic ambaye ni msemaji wa UNHCR, akizungumza leo Mjini Geneva amethibitisha kupata taarifa kutoka serikali ya Libya kuwa  zaidi wahamiaji 6,000 wamendelea kutekwa na  wahalifu katika maeneo mbalimbali nchini humo. Amesema   hii inafanya jumla ya idadi ya wahamiaji Sabratha kufikia  20,500, ikiwa ni pamoja na wale walio katika vituo vya uhamiaji.

UNHCR imekua mtari wa mbele kutoa misaada ya  dharura katika maeneo yote ambako wakimbizi na wahamiaji wamehamishiwa, na  wanaendela kufanya tathmini kuhusu  mahitaji mengine kwa wahamiaji hao.

Halikadhalika UNHCR imetoa malori 15  yaliyosheheni misaada ikiwa ni pamoja na mikeka ya kulala, magodoro,  vifa vya kujisafi  na blanketi za baridi.

Serikali ya Libya kwa kushirikiana na UNHCR na washirika wengine wanaendela kutoa misaada  mbalimbali ya dahurua japo uwezo wa kuwahudumia  ni mdogo ikilinganisha  na mahitaji ya wahamiaji  hao.