Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Utegemezi wa bidhaa unadhoofisha uchumi wa nchi zinazoendelea

Utegemezi wa bidhaa unadhoofisha uchumi wa nchi zinazoendelea

Kamati  Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo, UNCTAD imetoa ripoti leo mjini Geneva Uswis , ikihusu utegemezi wa nchi tisa zinazoendelea katika mauzo ya nje ya bidhaa kati ya mwaka 2010 na 2015,  na kufanya idadi ya nchi hizo kufikifkia  91, ambayo ni theluthi mbili ya nchi 135 zinazoendelea.

Hiyo ni kwa mujibu wa  ripoti ya Utegemezi wa mapato ya Serikali inaonyesha kwamba, nchi zinazoendelea zimeshuhudia mapato ya  mauzo yakiongezeka 25% hadi kufikia $dola trilioni 2.55.

Naye katibu mkuu wa UNCTAD Bw. Mukhisa Kituyi amesema, nchi zinazoendelea  zitakuwa na wakati mgumu kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu zisipoachana  na tabia ya  utegemezi wa bidhaa zinazosafirishwa nje.

Ameongeza kuwa utegemezi wa bidhaa unaweza kuathiri vibaya viashiria vya maendeleo ya kibinadamu kama vile umri wa kuishi, elimu, na mapato ya kila mtu,  kwa mujibu  ripoti ya utegemezi wa bidhaa ya 2016,  karibu theluthi mbili ya nchi zinazoendelea  zimerekodiwa katika kutegemea bidhaa zinazosafirishwa nje mwaka 2014 hadi 2015.

UNCTAD inafafanua kuwa nchi inafikia hatua ya kuwa tegemezi kwa bidhaa wakati bidhaa zake za kuuza nje zinachukua zaidi ya asilimia 60 ya mauzo ya jumla ya bidhaa.