ICRC yapunguza shughuli zake Afghanistan
Kamati ya kimataifa ya msalaba mwekundu ICRC, imeamua kupunguza shughuli zake nchini Afghanistan baada ya mfululizo wa mashambulizi dhidi ya wafanyakazi wake kaskazini kwa nchi hiyo.
Hii ni mujibu wa Monica Zanareli ambaye ni mkuu wa ujumbe wa ICRC nchini Afghanistan ambaye amesema tangu mwezi Disemba mwaka 2016 vituo vya ICRC kaskazini mwa Afghanistan, vimeshambuliwa mara 3.
Amesema baada ya majadiliano na makao makuu ya shirika hilo huko Geneva, ICRC sasa ofisi za ICRC huko Maimana na Kunduz zitagungwa na kupungunza uwakilishi wake huko Mazar-i-Sharif .
Bi Zanareli amesema uamuzi wa kupunguza shughuli zao Afghanistan umekua mgumu kwao baada ya miaka 30 ya huduma ya shirika hilo nchini.
Miongoni mwa visa vilivyokumba ICRC nchini Afghanistan ni pamoja na mfanyakazi wake kutekwa nyara mwaka 2016 huko Kunduz, na kuachiwa huru baada ya wiki 4.
Tukio hili lilifuatiwa na mauaji ya kikatili ya wafanyakazi sita kuchinjwa na wengine wawili kutekwa nyara katika jimbo la Jawzjan.