Neno la wiki: Utengamano na Utengano
Katika neno la wiki hii leo tunaangazia neno "Utengamano" na "Utengano". Mchambuzi wetu ni Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.
Nuhu anasema utengamano ni hali kuwa kwa pamojan au kushirikiana, na utengano ni kinyume cha utengamano, yaani hali ya kutokuwepo pamoja, iwe kimawazo au kiuhalisia...