Kimbunga Irma chaacha rekodi ya uharibifu
Tahadhari kuhusu kimbunga Irma iliyotolewa na kituo cha kitaifa cha hali ya hewa cha Marekani, na kituo cha dhoruba cha kitaifa kuhusu mafuriko, upepo wa mvua kalina dhoruba, inaonyesha kuwa Irma imesababisha uharibifu mkubwa katika maeneo mengi huko Florida.
Kituo hicho kimesema kimbunga Irma tayari kimesababisha uharibifu katika visiwa vya Caribean vilivyoko kwenye usawa wa bahari kama vile Kuba , uharibifu ulitokana na kimbunga hicho kuwa katikakiwango chadaraja la 5 .
Wataalamu hao wamelinganisha Irma kilichotokea Septemba 10 na kimbunga cha aina kama hiyo cha mwaka 1924 , eneo la Florida Marekani lieathirika zaidi na kimbunga hicho kilichiotua kikiwa katika daraja la 4 .
Licha ya dhoruba hiyo kupungua tarehe 11 septemba bado hali ni ya kutisha katika maeneo ya kusini mwa Florida ambapo thathmini ya madhila ya kimbunga hicho inategemewa kulingana na ile ya kimbunga harvey kilichotokea kusini mwa Huston Texas.