Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jukwaa kuhusu utatuzi wa changamoto za tabianchi lazinduliwa Addis Ababa

Jukwaa kuhusu utatuzi wa changamoto za tabianchi lazinduliwa Addis Ababa

Mashirika ya Umoja wa Mataifa yakiwemo WMO, UNDP, AFD, WFP kwa kushirikiana na banki ya maendeleo Africa  na Banki ya Dunia leo hii mjini Addis Ababa wamezidua jukwa la kwanza   la AMCOMET Africa Hydromet.

Jukwa hilo la aina yake  limewajumuisha  wajumbe 500 toka serikalini, sekta binafsi na asasi za kiraia za  mataifa  mbalimbali Africa ili kujadili mikakati ya mambo mbalimbali ikiwemo   Mafuriko, ukame, mlipuko wa kitropiki, na maporomoko ya ardhi yanayoendelea  na kusababisha uharibifu mkubwa na hasara Africa .

Naye makamu rais wa bank ya dunia Africa Bw. Makhtar Diop  amesema “Upepo wa kasi na ukubwa wa majanga ya asili kutoka kusini mwa Jangwa la Sahara unapaswa kuwa wito kwa  serikali na jumuiya ya kimataifa kuwekeza katika huduma za hydromet. Kuboresha usahihi wa utabiri wa hali ya hewa sio tu kuokoa maisha lakini pia kusaidia miji na jamii ya  Afrika kujenga ujasiri dhidi ya mabadiliko ya hali ya hewa.

Jukwaa litatoa miongozo kuhusu nguvu ya hydromet kama nguzo ya maendeleo ya hali ya hewa na ufanisi wa hali ya hewa.  Pia litaonyesha faida ya  hydromet katika sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na kilimo, maji, usafiri, anga ya anga, usimamizi wa rasilimali za asili, mazingira, nishati....Wajumbe katika  Jukwa  hilo watajitolea kutoa elimu  na  utekelezaji wa mikakati iliyopo pamoja na kupendekeza hatua halisi za kushughulikia hali ya hewa, maji, na changamoto za hali ya hewa inakabiliwa na Afrika.