Mjadala kuhusu umuhimu wa unyonyeshaji watoto Burundi
Ulimwengu umehitimisha wiki ya kunyonyesha juma hili, wataalamu wa shirika la afya ulimwenguni (WHO) wakichagiza kuwa faida za kunyonyesha sio tu kwa watoto lakini kwa jamii nzima hasa katika swala nzima la uzazi wa mpango.
Ingawa kinamama wazazi wengi wanachangamkia utaratibu huu wa kunyonyesha watoto, baadhi ya wanawake wamejenga hoja nyingi za kutonyonyesha watoto.
Burundi ni miongoni mwa nchi ambazo, serikali imeshikia bango suala la unyonyeshaji hasa miezi sita ya mwanzo mtoto akizaliwa.
Mwandishi wetu wa Maziwa Makuu Ramadhani KIBUGA amepita mtaani kujadili suala hili ungana naye.
(PKG YA RAMADHAN KIBUGA)