Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno la wiki: Rehani na Dhamana

Neno la wiki: Rehani na Dhamana

Katika neno la wiki hii leo tunaangazia maneno "Rehani" na "Dhamana" Mchambuzi wetu  ni Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha  Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.

Tukianza na Rehani, Bwana Zuberi anasema ukiwa na kitu ambacho unakipenda sana na unahitaji kukiweka rehani ili upate kitu kingine unachohitaji kama vile hela, inamaanisha kwamba utampelekea yule atakayekupa hela hizo kitu chako akiweke kisha unachukua hela, na utakapopata hizo hela unampelekea ili aweze kukurudishia kitu chako.  Na tukiangalia neno "Dhamana" ina maana ya kwamba ukiwa na mtu unayemfahamu kama rafiki na anaomba kitu chochote akiwa na mpango wa kulipa baadaye, na mwenye anamuomba hamfahamu, ukijitolea kumsimamia hadi atapoweza kulipa basi wewe umemwekea dhamana au umesimama kama shahidi, kiwango cha kwamba hata asipoweza kukilipia wewe mwenyewe utakilipia.