Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ukame watishia hali ya utulivu mjini Lafon, Sudan Kusini

Ukame watishia hali ya utulivu mjini Lafon, Sudan Kusini

Madhila ya watu nchini Sudan Kusini kufuatia ukame unaoikumba nchi hiyo ni muhimu yatatuliwe kwani huenda yakatishia amani inayoshuhudiwa katika baadhi ya maeneo ikiwemo kaunti ya Lafon. Kwa mujibu wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, UNMISS eneo hilo ni tulivu lakini hali ya kutegemea zao moja kwa kilimo limesababisha  hali kuwa mbaya zaidi kufuatia njaa Afrika Mashariki. Hata hivyo sasa kuna nuru gizani kwani mafunzo ya kulima mazao mbali mbali huenda yakasaidia kukabiliana na njaa, basi ungana na Grace Kaneiya katika makala ifuatayo.