Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kijana weka bunduki chini, chukua kalamu- Dor

Kijana weka bunduki chini, chukua kalamu- Dor

Kijana Dor Achek kutoka Sudan Kusini, alikuwa mkimbizi, aliyeishi katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya. Sasa kijana huyuni msomi na ana ndoto za kuwa balozi ili awasaidie wakimbizi hususani vijana.

Kijana huyu ambaye amehudhuria mkutano wa ngazi za juu kuhusu elimu amezungumza na Joseph Msami wa idhaa hii kumuelezea alikotoka,aliko na zaidi ya yote akiwataka vijana kuweka bunduki chini na kushika kalamu ili walete mabadiliko katika maeneo yenye migogoro.