Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wadau wakutana kujadili elimu jumuishi na yenye usawa

Wadau wakutana kujadili elimu jumuishi na yenye usawa

Mkutano wa ngazi ya juu kuhusu lengo namba nne la maendeleo endelevu SDGs linalotaka elimu jumuishi na yenye usawa pamoja na fursa kwa wote umeanza leo mjini New York Marekani, ukiwaleta pamoja wadau ili kutoa msukumo katika kutimiza lengo hilo. Flota Nducha na taarifa zaidi.

(TAARIFA YA FLORA)

Kwaya ya vijana kutoka Afrika Kusini ikitoa burudani yenye ujumbe kwa wadau hawa kabla ya kuanza kwa hotuba.

Miongoni mwa waliotoa hotuba zao ni Rais wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa aliyewataka wahudhuriaji kutumia fursa hiyo kuijenga dunia yenye mustakabali bora wa elimu.

(SFX)

Huyu ni Saul Mwame, mwanafunzi wa kidato cha nne shule ye sekondari DCT Mvumi mkoani Dodoma, Tanzania, ni miongoni mwa waliotoa hotuba katika kusanyiko hili.

Saul ni mwasisi wa taasisi ya kujenga mustakabali wa Afrika BAF, ambayo pamoja na membo mengine inawawezesha watu wenye ulemavu hususani vijana wanafunzi, ameiamba idhaa katika mahojiano maalum kwamba kilichomsukuma kuanzisha taasisi hiyo ni.

(Sauti Saul)

Anasema miongoni mwa matunda anayoshuhudia na kujivunia ni.

(Sauti Saul)