Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno la wiki: Hiba

Neno la wiki: Hiba

Wiki hii tunaangazia neno "Hiba" na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.

Bwana Sigalla anasema neno hiba lina maana mbili, moja ni kitu chochote anachopewa mtu kwa hiari au lengo la kuonyesha mapenzi, na lina maana sawa na idaya, adiya au azizi. Maana ya pili ni zawadi atoayo mtu kwa mpenzi au radhi ya mwenyezi Mungu kwetu.