Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nilitembea kutwa kucha na wanangu kutoka Sudan Kusini hadi Uganda kunusuru maisha-Sehemu ya 2

Nilitembea kutwa kucha na wanangu kutoka Sudan Kusini hadi Uganda kunusuru maisha-Sehemu ya 2

Kutana na Jade Kide katika sehemu ya pili ya mahojiano na John Kibego.  Yeye ni mama wa watoto wanne na amehaha kusaka hifadhi na kujikuta akitembea usiku na mchana kutoka Sudan Kusini kukimbia machafuko.

Amewasili Uganda katika kambi ya wakimbizi ya Kiryandongo, akiwa ametokea jimboni Equatoria Mashariki nchini Sudan Kusini. Anasilimulia kadhia zinazomakabili akikumbuka namna alivyompoteza mwanae na wazazi kufuatia mgogoro nchini mwake.