Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hatua za upasuaji kwa wagonjwa Fistula -sehemu ya kwanza

Hatua za upasuaji kwa wagonjwa Fistula -sehemu ya kwanza

Ugonjwa wa Fistula ambao huwakumba akina mama pindi wachelewapo kupata huduma wakati wa kujifungua ni changamoto hususan nchi zinazoendelea.

Hatua ya upasuaji dhidi ya wagonjwa wa Fistula hufanywa pale inapobidi kuokoa maisha ya mgonjwa. Katika sehemu ya kwanza ya makala ifuatayo Nicolaus Ngaiza wa redio washirika Kasibante Fm ya Kagera Tanzania anazungumza na Dk Martin Lwabilimbo kutoka idara ya upasuaji hospitali ya rufaa ya mkoa huo. Awali Dk Lwabilimbo anafafanua maana ya upasuaji huo.