Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno la Wiki: Mchapalo

Neno la Wiki: Mchapalo

Wiki hii tunaangazia neno "Mchapalo" na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.

Bwana Sigalla anasema mchapalo ni tafrija inayofanyika ambapo wahusika wanakunywa na kula wakiwa wamesimama na kubadilishana mawazo, kwa mfano katika sentensi "Mchapalo wa uzinduzi wa vitabu ulifana sana" inamaanisha kuwa watu walikuwa wakizungumza wakibadilishana mawazo huku wakiwa wanakula na kunywa..