Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nuru yaangazia familia za wakimbizi Ureno

Nuru yaangazia familia za wakimbizi Ureno

Familia kadhaa za wakimbizi kutoka Iraq na Palestina zimanufaika na ukarimu kutoka kwa moja ya miji nchini Ureno, ambapo mamlaka mjini humo imeonyesha ukarimu kwa kuwahifadhi na kukidhi haja zao.

Hatua hii inaunga mkono juhudi za Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR linalofanya kazi ya kulinda na kusaidia wale wanaokimbia vita na mateso tangu mwaka 1950.

Hadi sasa shirika hilo limefanikiwa kurejesha matumaini kwa mamilioni ya wakimbizi ulimwenguni kote.

Ungana na Amina Hassan katika makala ifuatayo kufahamu.