Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno la Wiki: SAKARANI

Neno la Wiki: SAKARANI

Wiki hii tunaangazia neno “Sakarani” na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.

Bwana Sigalla anasema neno Sakarani ni msamiati ya kawaida na lina maana tatu, la kwanza ni mtu asiye na akili timamu kutokana na ulevi, ya pili ni mtu ambaye amechanganyikiwa, yaani mwenye akili zisizosawa, na maana ya tatu ni mtu aliyetekwa akili zake kiasi kwamba anashindwa kuvumilia kwa sababu ya kupenda, kumaanisha mlevi wa mapenzi.