Neno La Wiki-Kizaazaa/ Tafrani/ Kizungumkuti
Neno la Wiki ambapo hii leo tunaangazia maneno Kizaazaaa, tafrani na kizungumkuti, Mchambuzi wetu ni Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA .
Bwana Nuhu anasema Kizaazaa ni hali ama mazingira na ni lazima kuwepo na shida, Tafrani ni hisia za mtu, hali ambayo sio ya kawaida na kizungumkuti ni neno linalotokana na mzunguko mzunguko wa kimawazo au hisia.