Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Zaidi ya watoto 150 wapoteza maisha Mediterranean mwaka huu-UNICEF

Zaidi ya watoto 150 wapoteza maisha Mediterranean mwaka huu-UNICEF

[caption id="attachment_316008" align="aligncenter" width="615"]dailynews081b-17

Zaidi ya watoto 150 wamepoteza maisha wakivuka bahari ya Mediterenia kutoka Afrika ya Kaskazini kuingia Italia mwaka huu. Hayo ni kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.

Hata hivyo shirika hilo linasema idadi kamili ya watoto walioathirika inaweza kuwa zaidi.

Tangu mwanzo wa mwaka huu karibu wakimbizi na wahamiaji 37 elfu ambapo asilimia 13 kati yao, wakiwa ni watoto, wamewasili Italia kupitia bahari ya Mediterranean, ikiwa ni ongezeko la asilimia 42 ikilinganishwa na wakati kama huu mwaka jana.