Ingawa kuna matumaini, hali bado ni tete Somalia na Sudan Kusini-UM
Hali ya kibinadamu nchini Somalia na Sudan Kusini bado ni tete kutokana na vita vinavyoendelea, ukame na maradhi.
Hayo yamesemwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa kutoka shirika la kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura (OCHA), shirika la idadi ya watu duniani (UNFPA) shirika la mpango wa maendeleo (UNDP) na shirika la kuhudumia watoto (UNICEF) uliozuru nchi hizo mbili kutathimini hali halisi.
Ujumbe huo ukizungumza na waandishi wa habari Jumanne mjini New York umesema hatua zimepigwa na wahudumu wa misaada ya kibinadamu kufikisha huduma na misaada inayohitajika kwa walengwa lakini bado kuna changamoto nyingi. John Ging ni mkurugenzi wa idara ya operesheni OCHA
(SAUTI YA JOHN GING)
Kwa upande wake Ugochi Daniels mkuu wa UNFPA kitengo cha masuala ya kibinadamu katika mazingira magumu amesema wanawake na watoto ndio wanaolipa gharama kubwa katika hali mbaya inayozikabili nchi hizo mbili
(SAUTI YA UGOCHI )
Naye mwakilishi wa UNDP Mburad Wahba amesema amejumuika na ujumbe huo kwenda Somalia na Sudan Kusini kuangalia jinsi gani suala la maendeleo linaweza kuchangia kupunguza makali ya hali ya sasa. Amesema UNDP imekuwa ikijishughulisha kwa kila hali hasa Somalia kuhakikisha mipango ya maendeleo kwa msaada wa wafadhili inapewa kipaumbele.