Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Washiriki wa #CPD50 wapaza sauti maswala ya afya

Washiriki wa #CPD50 wapaza sauti maswala ya afya

Mkutano wa 50 wa  kamisheni ya idadi ya watu na maendeleo wa Umoja wa Mataifa #CPD50 umeingia siku ya nne ambapo washiriki kutoka nchi mbali mbali wamekusanyika kwa ajili ya kujadili maswala ya ukuaji wa idadi ya watu na mienendo pamoja na ujumuishwaji wa ukuaji huo katika mikakati ya maendeleo.

Katika maswala ya idadi ya watu kunaibuka pia afya ya uzazi na usawa wa kijinsia na hizo ni baadhi ya mada ambazo zimejadiliwa hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, New York, Marekani. Basi ungana na Grace Kaneiya katika Makala hii na baadhi ya washiriki wa mkutano huo.