Neno la wiki- Misele
Katika neno la wiki hii leo tunaangazia matumizi yasiyo sahihi ya neno Misele Mchambuzi wetu Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA anasema neno misele ni aina ya dawa lakini linatumika kumaanisha kutia nakshi lakini hiyo si sahihi kwani hamna usanifu na lnatumika kwa mazoea lakini sio sanifu.