Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wanyamapori wainua vipato na elimu Uganda.

Wanyamapori wainua vipato na elimu Uganda.

Takwimu  za benki ya dunia za mwaka 2012 zinaonyesha kuwa Sekta ya utalii nchini Uganda huiliingizia taifa asilimia 3.7 ya pato la ndani  . Uwepo wa mbuga za wanyama ni sehemu ya mchango wa pato hilo.

Mbuga hizo za wanyama zimekuwa na manufaa kwa wakazi nchini humo hususani wale waishio jirani na mbuga za wanyama. Manufaa hayo sio tu ya kipato bali pia kielimu ambapo wanafunzi katika maeneo hayo wanasema wanyama huwasaidia katika masomo.