Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Upekee wa ushairi ni kwamba hutumia maneno teule-Walibora

Upekee wa ushairi ni kwamba hutumia maneno teule-Walibora

Katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya ushairi, shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni,  UNESCO limesema kwamba ushairi unalenga ubinadamu na maadili ya watu wote na kwamba kubadilisha shairi jepesi kuwa kichocheo thabiti kwa ajili ya kuibua majadiliano na kuleta amani.

UNESCO inasema kuwa ushairi kama fasihi, ni dirisha linalotoa fursa ya kuonyesha tofauti miongoni mwa binadamu. Kwa upande wake mshairi, na mwandishi mashuhuri kutoka Kenya, Ken walibora anasema ushairi ni kama fasihi nyingine lakini upekee wake ni matumizi ya maneno mateule, je ni kwa vipi? Grace Kaneiya amezungumza naye na bila shaka akaanza na kughani moja ya mashairi yake.