Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkutano wa 61 wa kamisheni ya hadhi ya wanawake CSW61 waangaziwa

Mkutano wa 61 wa kamisheni ya hadhi ya wanawake CSW61 waangaziwa

Mkutano wa 61 wa kamisheni ya hadhi ya wanawake umeanza tarehe 13 mwezi huu wa Machi kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Asasi za kiraia kutoka sehemu mbalimbali zinazojihusiha na masuala ya ustawi wa wanawake zimewakilishwa huku pia serikali zikituma wawakilishi wake kushiriki katika mikutano mbalimbali ya ndani kuhusu masuala ya wanawake. Je nini kilijiri?