Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno la Wiki- Gozigozi

Neno la Wiki- Gozigozi

Katika neno la wiki hii leo tunaangazia matumizi yasiyo sahihi ya neno gozigozi. Mchambuzi wetu  Nuhu Zubeir Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha  Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA anasema neno gozigozi linatumiwa likimaanisha upuuzi au mambo ya hovyo. Lakini kimsingi neno gozi linamaanisha ngozi ya mnyama iliyochunwa na kuachwa hadi ikaoza na pia maana yake nyingine inakwenda katika lugha za kitamaduni. Je ni ipi hiyo? msikilize basi maelezo yake.