Neno la wiki- Jabari
Wiki hii tunaangazia neno Jabari na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.
Bwana Sigalla anasema neno hili lina maana zaidi ya moja, maana ya kwanza ni mtawala mkuu wa pekee, maana ya pili ni mtu shujaa asiye na woga na maana ya tatu ni jeuri.