Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kuelekea 2030, wanawake wamejizatiti kufikia #5050

Kuelekea 2030, wanawake wamejizatiti kufikia #5050

Tarehe Nane mwezi Machi, kwa zaidi ya karne moja sasa, imekuwa ni siku  ya kuadhimisha siku ya wanawake duniani. Siku hii ikiangazia harakati za kuweka usawa wa kijinsia kwa mustakhbali bora siyo tu wa kundi hilo ambalo ni zaidi ya asilimia 50 duniani, bali pia kwa ulimwengu wote kwani wahenga walisema ukimwendeleza mwanamke umeendeleza jamii nzima.

Sasa katika maadhimisho haya tumetathmini hali ya mwanamke kiuchumi, kisiasa na kijamii na mwelekeo wa usawa wa 50 kwa 50 ifikapo mwaka 2030 katika mazingira ya sasa ya kazi ulimwenguni yanayobadilika.