Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Burudani zasheheni wakati wa kuadhimisha siku ya wanawake duniani.

Burudani zasheheni wakati wa kuadhimisha siku ya wanawake duniani.

Wanawake wameshamiri juma hili. Mataifa mengi yameadhimisha siku ya wanawake duniani mnamo Machi nane, siku ambayo huadhimishwa kila mwaka, lengo likiwa kupigia chepuo haki na ustawi wa kundi hilo katika nyanja mbalimbali.

Katika makala ifuatayo Assumpta Massoi anamulika namna burudani ilivyotumiwa kufikisha ujumbe hususani nchi zenye mizozo, huku ikiwaliwaza washiriki, wakiongozwa na wanawake ambao ni walengwa.