Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tukipata teknolojia wezeshi tutazalisha maradufu: Wajasiriamali Wanawake

Tukipata teknolojia wezeshi tutazalisha maradufu: Wajasiriamali Wanawake

Ukosefu wa teknolojia wezeshi unapunguza mapato kusudiwa kwa wanawake mkoani Kagera nchini Tanzania, hii ni kwa mujibu wa wajasiriamali mkoani humo ambao wanasema wakiwezeshwa kiteknolojia watazalisha maradufu.

Nicolaus Ngaiza wa redio washirika Kasibante Fm ya Kagera nchini humo, amevinjari hadi wajasiriamali hao wanawake wanapofanya kazi zao ili kujionea. Ungana naye katika makala ifuatayo.