Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno la Wiki- Madhabahu

Neno la Wiki- Madhabahu

Wiki hii tunaangazia neno "Madhabahu" na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.

Bwana Sigalla anasema neno hilo lina maana tatu. Maana ya kwanza ikiangazia pahala takatifu, maana ya pili ni pahala pa kufanyia tambiko na maana ya tatu ni pahala pa kuchinjia wanyama.