Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Redio imerahisisha mawasiliano miongoni mwetu: Wakimbizi

Redio imerahisisha mawasiliano miongoni mwetu: Wakimbizi

Wakimbizi wawapo kambini huendelea na maisha kama jamii nyingine, hivyo huhitaji mawasiliano ya mtu na mtu na makundi mengine ya kijamii. Mchakato wa mawasiliano hukabiliwa na vikwazo kama vile kuchelewa kwa ujumbe au kutofika kabisa. Ndiposa redio kama chombo cha habari hutumika kuwafikishia taarifa tofautitofauti na kuwaelimisha kuhusu mambo yawahusuyo.

Katika mfululizo wa makala leo tunamulika umuhimu wa redio kwa wakimbizi walioko Kigoma Tanzania, ambapo Kongolo Mubanga Kahenga wa redio washirika redio Umoja ya Kigoma Tanzania anazungumza na kundi hili.