Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Radio ni tegemeo katika kuendesha shughuli za kipato Tanga, Tanzania

Radio ni tegemeo katika kuendesha shughuli za kipato Tanga, Tanzania

Radio ambayo ni chombo cha mawasiliano inatajwa kuwa muhimu katika kutoa taarifa iwe ni habari kuhusu matukio mbali mbali ulimwenguni au taarifa kuhusu bei ya vyakula sokoni au hali ya hewa. Taarifa kama hizi ni muhimu kwa jamii husika kwani zinatumika katika kuendesha kazi za kila siku, mathalani kilimo au uvuvi.

Umuhimu wa radio katika nyanja hizo umedhihirika katika makala hii ya Martha James wa radio washirika Pangani FM kutoka Tanga nchini Tanzania.