Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vijana wana fursa katika utatuzi wa migogoro na kukuza maendeleo: Siniga

Vijana wana fursa katika utatuzi wa migogoro na kukuza maendeleo: Siniga

Baraza la vijana la Umoja wa Mataifa hivi karibuni limekutana hapa makao makuu ya umoja huo mjini New York, katika kongamano la kujifunza namna chombo hicho kinavyofanya kazi na kutatua changamoto kadhaa za dunia.

Miongoni mwa washiriki ni Paul Siniga ambaye ni balozi wa vijana wa Umoja wa Mataifa wa Tanzania, ambaye ameiambia idhaa hii katika mahojiano maalum kuwa kongamano hilo limetoa fursa ya kujifunza utatuzi wa changamoto za dunia kama vile.

( Sauti Siniga)

Kijana huyu ambaye ni mjasiriamali katika mitindo anasema vijana wana nafasi kubwa katika ujenzi wa maendeleo na amani kwani.

( Sauti Siniga)