Kongamano la vijana kuhusu maendeleo endelevu
Juma hili katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani, kumefanyika kongamano la tano la baraza la uchumi na kijamii la Umoja wa Mataifa, ECOSOC kuhusu vijana, ambao liliangazia nafasi ya vijana katika utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, SDGs
Kongamano hilo limewaleta pamoja zaidi ya vijana 800 kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, ambapo kwa siku mbili wameshiriki mijadala ya kubadilishana uzoefu na mbinu mujarabu za kuitokomeza umasikini.
Kufahamua kwa undani mitizamo ya washiriki,tuungane na Assumpta Massoi