Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Utamaduni wa Oromo uliotambuliwa na UNESCO

Utamaduni wa Oromo uliotambuliwa na UNESCO

Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO linaendeleana kazi yake ya kubaini tamaduni za aina yake ulimwenguni ambazo zinapaswa kuhifadhiwa ili ziweze kuendelea kurithiwa kizazi na kizazi. Mojawapo ni mfumo wa kisiasa, kiuchumi na kijamii wa kabila la Oromo nchini Ethiopia. Mfumo huo wa maisha unarithishwa kwa njia ya simulizi na tayari UNESCO umeingiza katika orodha ya turathi za tamaduni zisizogusika za kibinadamu. Je ni aina gani? Assumpta Massoi anasimulia kwenye makala  hii.