Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Asilimia 81 ya watoto hubwetesha miili yao-WHO

Asilimia 81 ya watoto hubwetesha miili yao-WHO

Ukosefu wa kazi zainazohusisha viungo vya mwili ni moja ya vigezo vikuu vya hatari ya magonjwa yasiyoambukiza ( NCDs), limesema leo shirika la afya ulimwenguni, WHO.

Katika chapisho la shirika hilo kuhusu hatari ya kupata magonjwa hayo, WHO imesema kuwa magonjwa hayo kama vile kiharusi, kisukari na saratani yanasababishwa kwa asilimia kubwa na kudorora kwa miili kunakotokea katika nchi nyingi.

Kwa mujibu wa WHO, duniani kote asilimia 81 ya watoto wanaopaswa kuwa shule hawafanyi shughuli za kufanya viungo vya mwili vihusike na kuchangamka na badala yake wanabweteka.

Kazi hizo zinasaidia kuboresha afya ya mwili na ni vyema zikafanyika mara kadhaa na kuepuka kutofanya lolote kwa muda mwingi, limeshauri shirika hilo la afya ulimwenguni.