Nuru yamwangazia mtoto mkimbizi kutoka Syria
Mtoto Mohammed ambaye alizaliwa na uziwi, ni mkimbizi nchini Lebanon, akiwa na miaka minane tu amepitia changamoto nyingi katika maisha yake mafupi. Lakini nuru imemwangazia kwani kupitia shule moja nchini humo sasa amepata sauti na mustakhbali wake una mwanga, basi ungana na Selina Jerobon Kwa undani wa makala hii.