Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baada ya kilio ni faraja kwa familia iliyokimbilia Ubelgiji

Baada ya kilio ni faraja kwa familia iliyokimbilia Ubelgiji

Wahamiaji ambao wanajaribu kuvuka bahari ya mediteranea wanakabiliwa na hatari kubwa katika safari zao. Mmoja wa wahanga wa hatari ni mtoto Dina ambapo akiwa na umri wa miezi minne tu akiwa katika nyumba ya msafirishaji haramu nchini Libya aliungua na kupata majeraha kwa asilimia 80 ya mwili wake. Baada ya zaidi ya mwaka mmoja wazazi wake wanatafakari ajali hiyo ambayo huenda ingawalipokonya uhai wa  mtoto wao.Basi ungana na ….. katika makala hii ya wahamiaji walioko Ubelgiji.