Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Harakati za kuimarisha Kiswahili zashika kasi Uganda

Harakati za kuimarisha Kiswahili zashika kasi Uganda

Nchini Uganda harakati zinaendelea ili kufanikisha azma ya serikali ya kupanua matumizi ya lugha ya Kiswahili. Harakati hizo ni pamoja na shule za msingi kuchukua hatua kuwapatia wanafunzi stadi mbali mbali za kufanikisha mpango huo wakati huu ambapo Kiswahili ni moja ya lugha rasmi za Muungano wa Afrika, AU. Je nini kinafanyika? Ungana na John Kibego kwenye makala hii kutoka Hoima, Uganda.