Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNAMI yalaani utekaji wa mwandishi wa habari huko Iraq

UNAMI yalaani utekaji wa mwandishi wa habari huko Iraq

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Iraq (UNAMI) umelaani utekaji wa mwandishi wa habari wa Iraq, Bi Afrah Shawqi, na watu wenye silaha wasiojulikana kutoka nyumbani kwake Jumatatu usiku Desemba 26.

UNAMI imeitaja kuwa shambulizi kubwa juu ya uhuru wa kujieleza nchini ikisema kuwa uhuru ni jambo la msingi kwa jamii zote za kidemokrasia na lazima kuheshimiwa wakati wote na katika hali zote.

Ujumbe huo umetoa wito kwa wahusika kumuachilia huru na kwamba mamlaka ya kuchunguza na watakopatikana na hatia sheria kuchukuliwa haraka iwezekanavyo.