Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Misaada ya vyakula yaanza kuwafikia wakazi wa Aleppo

Misaada ya vyakula yaanza kuwafikia wakazi wa Aleppo

Baada ya vuta nikuvute baina ya pande kinzani nchini Syria juu ya kuruhusu watoa misaada ya kibinadamu mjni Aleppo, mji unaotajwa kuathirika zaidi na mzozo nchini humo, hatimaye wakazi wa mji huo hususani Mashariki wameona nuru kwa kupata misaada ya vyakula.

Umoja wa Mataifa umeanza operesheni ya kugawa vyakula katika mji huo ambao umezingirwa na vikosi vyenye silaha. Joseph Msami amemulika kuanza kwa ugawaji huo na hii hapa ni taarifa yake.