Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkate na maji ndio tegemeo Haiti

Mkate na maji ndio tegemeo Haiti

Tangu kimbunga Matthew kipige Haiti tarehe Nne Oktoba mwaka huu, shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF limesema bado mamia ya maelfu ya mamia ya watoto nchini humo hawana makazi wala chakula, hawaendi shule na wamo hatarini. Kimbunga hicho kilichoporomosha majengo, na kusomba mimea na miondombinu kimeacha nchi hiyo masikini katika hali mbaya zaidi. Mmoja wa waathirika ni mtoto mwenye umri wa miaka 15 na katika makala hii anatusimulia kile anachokipitia. Basi ungana na Flora Nducha kufahamu zaidi...