Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watu wenye ulemavu Tanzania wataka mtandao wa kupaza sauti zao

Watu wenye ulemavu Tanzania wataka mtandao wa kupaza sauti zao

Umoja wa Mataifa unasema watu wenye ulemavu wanahitaji kupewa kipaumbele katika sera, mipango na huduma mbalimbali ili wajumuishwe katika ajenda ya maendeleo endelevu ya mwaka 20130 ambayo nchi wanachama wa umoja wa huo zinapaswa kutimiza.

Nchini Tanzania kundi hilo linapigia chepuo juhudi za mtandao wa kuwasaidia watu wenye ulemavu . Ni hatua zipi wanazochukua? Ungana na Tumaini Anatory  wa redio washirika Karagwe Fm ya Kagera Tanzania.