Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ukitaka ujuzi anza kujitolea: Aloo

Ukitaka ujuzi anza kujitolea: Aloo

Kujitolea hukuza ujuzi, lakini pia huleta utoshelevu, ni maneno ya mbobezi katika kujitolea ambaye ni Afisa Programu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kujitolea UNV nchini Tanzania Josep Aloo katika mahojiano na Afisa wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa nchni humo Stella Vuzo.

Bwana Aloo ambaye anaratibu maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kujitolea Disemba tano, kwa Tanzania, amesema jamii bado ina uelewa mdogo kuhusu kujitolea jambo linalohitaji kupigiwa upatu zaidi.

Hapa anaanza kwa kueleza kitakaochofanyika mwishoni mwa juma katika kuienzi siku hiyo adhimu.