Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno la Wiki- Mende

Neno la Wiki- Mende

Katika neno la wiki Disemba 2 tunachambua neno Mende, mchambuzi wetu leo ni, Nuhu Zuberi Bakari ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha  Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.

Bwana Bakari anasema mende ni jamii ya mdudu ambaye amegawanyika kwa sehemu tatu, mende huyo anachukua majina tofauti kulingana na mazingira aliyomo, kombamwiko akiwa jikoni, akiwa kwenye sehemu chafu ni mende na akiwa ni wa kike amebeba mayai ni nyenze.