Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ujauzito utotoni nchini Tanzania

Ujauzito utotoni nchini Tanzania

Siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake zinamulikwa hivi sasa ulimwenguni kote. Wanawake na wasichana hususan katika nchi zinazoendelea hukatiliwa kwa njia mbali mbali, na hawana pa kukimbilia kwani sheria mbovu nazo haziwapi ulinzi wa aina yoyote,  na matokeo yake hali hii huzorotesha maendeleo yao.  Katika makala ifuatayo tunakupeleka nchini Tanzania kupata moja ya mifano mingi ya ukatili dhidi ya wanawake. Basi tuungane na Amina Hassan.