Muziki unaleta pamoja itikadi, dini na imani tofauti: Sheilla
Kutana na Sheilla Akwara, mwanamuziki kutoka Kenya anayeng’ara katika muziki wa injili.
Mwanamuziki huyu ambaye amekuwa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York kwa miezi kadhaa akifanya mafunzo ya kazi, anatumia muziki wake kuelimisha jamii katika mambo mbalimbali ikiwamo amani na utengamano. Fuatana na Joseph Msami katika makala inayomulika kipaji cha Sheilla .