Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tushikamane na ishara ndogo ya matumaini Sudan Kusini: Løj.

Tushikamane na ishara ndogo ya matumaini Sudan Kusini: Løj.

Ni lazima kusalia katika ishara ndogo ya matumaini, amesema Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nhini Sudan Kusini na mkuu wa ujumbe wa umoja huo nchini humo UNMISS Ellen Margarethe Løj.

Katika mahojiano maaulum na redio ya Umoja wa Mataifa na idhaa hii, kiongozi huyo anayemaliza muda wake wa uongozi, amesema hali ya kibinadamu ni mbaya lakini alipoulizwa kama kuna dalili yoyote ya matumaini akasema.

( SAUTI LOJ)

‘‘Huwezi kuwa mkuu wa ujumbe wa kulinda amani nchiniSudan Kusini na usishikamane na ishara ndogo ya matumaini. Inaonekana ngumu sana, na ni ngumu hakika. Hatuwezi kukata tamaa, kwasababu tukikata tamaa, ni watu wa Sudan Kusini ambao wanateseka.’’

Bi Løj hapo jana amelihutubia baraza la usalama ambapo pia amesema viongozi wa tiafa hilo wanapaswa kuweka maslahi ya taifa mbele kwa kutekeleza mkataba wa makubaliano ya amani